Sunday, May 17, 2015

MINYOO YA KUKU (2)

ATHARI ZA MINYOO KWA KUKU

Minyoo kwa kuku ina athari nyingi, athari ambazo zinaweza hadi kumpatia hasara mfugaji kama hatozingati ratiba ya kuwapa dawa ya minyoo kuku wake kila baada ya miezi mitatu. Athari za minyoo kwa kuku ni kama zifuatazo:-
Minyoo mara zote ndani ya mwili wa kuku hutumi virutubisho ambavyo tayari vishameng'enywa na kuku, hali ambayo humfanya kuku kushindwa kurudisha au kufidia nguvu (digestible energy)  aliyoipoteza katika kumeng'enya chakula, atashindwa pia kupata virutubisho vya ukuaji (nutrients  for growth) , na kama haitoshi pia atakosa kupata virutubisho vya uzalishaji (nutrients for production), hali ambayo itamfanya kuku kudhoofika, kudumaa, kupunguza au kutotaga kabisa na hatimaye kufa.

No comments:

Post a Comment