Friday, August 1, 2014

KIPINDUPINDU CHA KUKU (FOWL CHOLERA)

KIPINDUPINDU CHA KUKU (FOWL CHOLERA)

 Ni ugonjwa unaosababishwa na bacteria ambao unaoshambulia karibu aina zote za ndege, ugonjwa huu ni hatari ambapo vifo ni kati ya 30% hadi 80%.

Njia za ueneaji ugonjwa

  • Utupaji ovyo wa mizoga ya kuku, kwani mzoga unaweza kukaa na vimelea kwa zaidi ya miezi mitatu.




  • Kupitia chakula na maji yenye mchanchanyiko na vimelea hivyo.
  • Kuku mzima kugusana na kuku mgonjwa.
  • Kupitia njia ya upumuaji.  

Dalili za Fowl Cholera

  • Huarisha majimaji ya kijani yenye harufu.


  • Kilemba na masikio ya kuku hupauka na kulegea.


  • Hupumua kwa shida.


  • Hutokwa na ute mdomoni na puani.


  • Joto la mwili hupanda.


  • Vifo hutokea  


 Jinsi ya Kudhibiti Fowl Cholera

  • Usafi wa ndani na nje ya banda.
  • Tenganisha kuku kwa rika zao (wakubwa kwa wakubwa na wadogo kwa wadogo).
  • Zingatia sifa za banda bora.
  • Mizoga ichomwe moto au ifukiwe katika shimo la kina kirefu kuzuia kuenea kwa ugongwa.  

Tiba ya Fowl Cholera

Ukiona dalili za ugonjwa huu wahi mapema kutumia dawa mojawapo kati ya zifuatazo:~
  1. Trimazin
  2. Typhoprim
  3. Sulphonamides
  4. Hipraloma
  5. O.T.C
  6. C.T.C 
  7. Ganadex   

No comments:

Post a Comment