Wednesday, October 14, 2015

MAFUNZO KWA VITENDO

SIFA ZA JOGOO NA TETEA BORA

1. SIFA ZA JOGOO BORA

  • Awe na umbo kubwa
  • Awe na ukiko nzuri usioangukia upande mmoja
  • Awe mchangamfu
  • Apende kuwa na himaya yake. Sifa hii utaigundua pindi ukimjazia wapinzani, atakuwa anapigana badala ya kufuata matetea.



2. SIFA ZA TETEA BORA

  • Awe na umbo kubwa
  • Awe na uwezo wa kuatamia
  • Awe na uwezo wa kulea vizuri (high mothering ability)
  • Aweze kutaga mayai ya kutosha.

DARASA LA UFUGAJI

LISHE BORA ENDELEVU KWA MATOKEO BORA ZAIDI

Mfugaji ili uwape kuku wako lishe bora yenye kuendelea, na ili upate matokeo bora zaidi katika ufugaji wako wa kuku basi yakupasa kuzingatia yafuatayo:-
  • Tumia chakula bora na siyo bora chakula. Tumia chakula bora ambacho hakina madhara kwa kuku wako na hata walaji kwa ujumla.
  • Weka chakula mahali safi na salama kuepuka wadudu waharibifu kama vile panya ili kuzuia maambukizi ya magonjwa kwa kuku.
  • Tumia kanuni ya "least cost combination" yaan tumia chakula cha bei nafuu kinachotoa matokeo bora zaidi ili kupunguza gharama za ufugaji hali ambayo itakufanya upate faida mara dufu.
Kwa kufanya hivyo utaweza kuwalisha kuku wako chakula kilicho bora kwa matokeo bora zaidi bila kuyumba kiuchumi wakati wote wa ufugaji wako.

Thursday, October 8, 2015

MAFUNZO KWA VITENDO

SIFA ZA JOGOO NA TETEA BORA

1. SIFA ZA JOGOO BORA
  • Awe na umbo kubwa
  • Awe na ukiko nzuri usioangukia upande mmoja
  • Awe mchangamfu
  • Apende kuwa na himaya yake. Sifa hii utaigundua pindi ukimjazia wapinzani, atakuwa anapigana badala ya kufuata matetea.
2. SIFA ZA TETEA BORA

  • Awe na umbo kubwa
  • Awe na uwezo wa kuatamia
  • Awe na uwezo wa kulea vizuri (high mothering ability)
  • Aweze kutaga mayai ya kutosha.

ATHARI ZA KIMAZINGIRA KATIKA ULAJI WA KUKU

Kuna sababu mbalimbali zinazoathiri ulaji wa kuku, athari hizo zinaweza zikamfanya kuku ale sana au asile kabisa. Zifuatazo ni sababu za kimazingira zinazoathiri ulaji wa kuku:-
1. JOTO
Ulaji wa chakula hupungua kadri joto la mazingira linavyoongezeka, kwan kama tujuavyo zoezi la umeng'enyaji wa chakula huongeza joto la mwili, na joto la mwili halitakiwi kupanda wala kupungua, hivyo basi ubongo unamuamuru kuku asile ili kudhibiti joto la mwili lisipande.

Angalizo ni kwamba mfugaji anatakiwa achunge hali ya joto la banda, kwan hata akizidisha balbu au banda likikosa hewa ya kutosha pia inaweza kusababisha joto la mazingira kuongezeka na kupelekea kuku kukosa hamu ya kula hali amabayo itawafanya kuku wadumae.

2. BARIDI
Kipindi cha baridi kuku wanakula sana kwa sababu ubongo unamuamuru kuku ale sana kwa kuwa umeng'enyaji unatakiwa uwe mara kwa mara ili kudhibiti joto la mwili lisishuke.

3. MHEMUKO (STRESS)
Banda likiwa chafu, au lipo sehemu yenye kelele za mara kwa mara, au umeweka kuku wengi katika banda dogo itawasababishia kuku kupata stress hali ambayo itawafanya kuku wakose hamu ya kula.

4. UPATIKANAJI WA MAJI
Maji yanakazi kubwa sana katika umeng'enywaji wa chakula (digestion process), kwa hiyo kuku ukiwabania maji na ulaji wao pia utapungua, kwani zoezi la umeng'enyaji chakula utakuwa unafanyika taratibu sana hali ambayo itawafanya kuku kukaa muda mrefu bila kuhitaji chakula.

5. MUUNDO WA VYOMBO VYA CHAKULA NA MAJI
Muundo mbovu wa vyombo vya chakula na maji utasababisha chakula au maji kuchanganyika na vitu visivyofaa (feed or water contamination) kama vile kinyesi hali ambayo itapunguza ulaji wa kuku.

Friday, September 25, 2015

MAFUNZO KWA VITENDO

MADHARA YA KUACHA BANDA CHAFU

Katika ufugaji kitu kikubwa na muhimu kuzingatia ni usafi, bila usafi hata uwe unawapatia chakula aina gani kuku hawawezi kufanya vizuri. Yafuatayo ni madhara yapatikanayo kwa kuacha banda chafu:-

1. MRUNDIKANO WA VIJIDUDU VYA MAGONJWA
Kama tujuavyo banda likiwa chafu kunakuwa na mazalia ya vijidudu vya magonjwa kama vile kuhara damu (coccidiosis), homa ya matumbo (typhoid) na mafua, magonjwa ambayo yanaweza kusababisha vifo vingi katika banda lako na kupelekea kupata hasara.

2. KUKU KUDUMAA NA KUPUNGUZA UTAGAJI
Kuku wakiwa katika ugonjwa wowote dalili ya kwanza kabisa ni kupoteza hamu ya kula hali ambayo inawapelekea kudumaa kwa kukosa lishe bora. Na kwa upande wa kuku wa mayai huwa wanapunguza kutaga au kutotaga kabisa kwa kukosa nguvu ya kuzalishia (production energy).

3. "STRESS " KWA MFUGAJI
Mfugaji anaweza kupata mhemuko (stress) kutokana na kutibu mara kwa mara bila mafanikio kwa magonjwa yaleyale kujirudia, na wingi wa vifo vitavyokuwa vinatokea kila siku.

Friday, September 11, 2015

DARASA LA UFUGAJI

ZINGATIA HAYA ILI UPATE FAIDA ZAIDI

Baada ya kuwa mfugaji amefuata taratibu zote katika ufugaji wake wa kuku kwa lengo la kupata faida, Ili mfugaji huyo apate faida zaidi kuna mambo muhimu ya kuzingatia hususan katika kujenga soko lake kama ifuatavyo:-


1. Lenga soko sikukuu za mwisho wa mwaka na zinginezo ambapo kuku huuzwa zaidi.
2. Tafuta masoko ili ujenge jina kwa wanunuzi wakubwa.
3. Jiunge au shirikiana na wenzako kuunda kikundi cha wafugaji (wafuga kuku) ili muweze
  • Kuchanja pamoja kupunguza gharama (kwa wafugaji wadogo)
  • Kutafuta masoko pamoja
  • Kupasiana wateja kama hauna kuku wakati huo
4. Kuweza kujitambulisha katika masoko kwamba Kijiji au kikundi chenu kuku wanapatikana muda wote

Tuesday, August 25, 2015

MAFUNZO KWA VITENDO

MAMBO YA KUJIEPUSHA NAYO KATIKA UFUGAJI

Ndugu mfugaji ni ukweli usiopingika wala kujadilika kuwa katika ufugaji kuna baadhi ya mambo wafugaji tunayafanya lakini hayakupaswa kufanyika, yafuatayo ni ya kujiepusha nayo katika ufugaji:-

  • Kuacha banda chafu
  • Kuleta kuingiza kuku wageni bila kujua historia ya chanjo walipotoka.
  • Kuuza kuku wagonjwa.
  • Kuchinja kuku wagonjwa.
  • Kununua kuku wagonjwa.
  • Kutupa kuku waliokufa porini.
  • Kununua chanjo kwa wauzaji wanaofahamika kuwa hawana solar power au jenereta.
  • Kutibu kwa mazoea bila kuwasiliana na Afisa Mifugo.
  • Kutembelea mabanda ya jirani bila kuchukua tahadhari.

Sunday, August 9, 2015

DARASA LA UFUGAJI

FIKIRIA KIKUBWA ANZA NA KIDOGO

Hii ni kwa wote, wafugaji na wanaotaka kuanza kufuga. Unapotaka kuanza ufugaji unatakiwa uanze na ufugaji mdogo hatakama una mtaji mkubwa. Kwa kufanya hivi itakusaidia kupata uzoefu katika nyajna zifuatazo:

1. UTUNZAJI (MANAGEMENT)
Kwa kuanza na kiasi kidogo itakusaidia kujua ni ukubwa gani unafaa kwa kuku wangapi, ukiwa na kuku wangapi utalisha chakula kiasi gani, pia utapata uzoefu wa chanjo muhimu zinazohitajika hali ambayo itakurahisishia pindi utapoanza ufugaji mkubwa.

2. SOKO
Hapa tunalenga upatikanaji wa wateja wa bidhaa zako za mifugo, itakusaidia kujua wateja waliopo wanavutiwa na bidhaa ya aina gani, kwa mfano mayai utajua wanapenda mayai ya kiini cheupe au cha njano? Kwa kufaham wanchokihitaji utajua ufanye nini ili ukidhi wanachokihitaji.

3. CHANGAMOTO
Ukianza na ufugaji mdogo pia itakusaidia kujua changamoto zilizopo kwenye ufugaji na utajifunza ni jinsi gani ya kuzitatua au kukabiliananazo kabla  ya kuanza ufugaji mkubwa.