Friday, September 25, 2015

MAFUNZO KWA VITENDO

MADHARA YA KUACHA BANDA CHAFU

Katika ufugaji kitu kikubwa na muhimu kuzingatia ni usafi, bila usafi hata uwe unawapatia chakula aina gani kuku hawawezi kufanya vizuri. Yafuatayo ni madhara yapatikanayo kwa kuacha banda chafu:-

1. MRUNDIKANO WA VIJIDUDU VYA MAGONJWA
Kama tujuavyo banda likiwa chafu kunakuwa na mazalia ya vijidudu vya magonjwa kama vile kuhara damu (coccidiosis), homa ya matumbo (typhoid) na mafua, magonjwa ambayo yanaweza kusababisha vifo vingi katika banda lako na kupelekea kupata hasara.

2. KUKU KUDUMAA NA KUPUNGUZA UTAGAJI
Kuku wakiwa katika ugonjwa wowote dalili ya kwanza kabisa ni kupoteza hamu ya kula hali ambayo inawapelekea kudumaa kwa kukosa lishe bora. Na kwa upande wa kuku wa mayai huwa wanapunguza kutaga au kutotaga kabisa kwa kukosa nguvu ya kuzalishia (production energy).

3. "STRESS " KWA MFUGAJI
Mfugaji anaweza kupata mhemuko (stress) kutokana na kutibu mara kwa mara bila mafanikio kwa magonjwa yaleyale kujirudia, na wingi wa vifo vitavyokuwa vinatokea kila siku.

No comments:

Post a Comment