Friday, September 11, 2015

DARASA LA UFUGAJI

ZINGATIA HAYA ILI UPATE FAIDA ZAIDI

Baada ya kuwa mfugaji amefuata taratibu zote katika ufugaji wake wa kuku kwa lengo la kupata faida, Ili mfugaji huyo apate faida zaidi kuna mambo muhimu ya kuzingatia hususan katika kujenga soko lake kama ifuatavyo:-


1. Lenga soko sikukuu za mwisho wa mwaka na zinginezo ambapo kuku huuzwa zaidi.
2. Tafuta masoko ili ujenge jina kwa wanunuzi wakubwa.
3. Jiunge au shirikiana na wenzako kuunda kikundi cha wafugaji (wafuga kuku) ili muweze
  • Kuchanja pamoja kupunguza gharama (kwa wafugaji wadogo)
  • Kutafuta masoko pamoja
  • Kupasiana wateja kama hauna kuku wakati huo
4. Kuweza kujitambulisha katika masoko kwamba Kijiji au kikundi chenu kuku wanapatikana muda wote

No comments:

Post a Comment