Monday, May 18, 2015

DARASA LA UFUGAJI

FAIDA ZA UFUGAJI KUKU

Tunafaham kuwa unajua faida za kuku lakini ngoja tukumbushe yafuatayo kuhusu faida za ufugaji kuku.
  • Kuku ni chanzo cha haraka cha pesa kwa kuuza kuku au mayai.
  • Kuku wanaweza kabisa kukuongezea kipato na kukuondolea kabisa umaskini.
  • Nyama ya kuku na mayai ni protini muhimu kwa familia, yaan watoto, wagonjwa na hata wazee.
  • Kinyesi cha kuku pia ni mbolea, lakini kama haitoshi maganda ya mayai na manyoya ni mapambo.
  • Hakuna dini wala utamaduni wowote Tanzania unaozuia kula kuku.
  • Katika nyama ambayo haina madhara yoyote katika mwili wa binadamu ni nyama ya kuku na samaki.
  • Ni mradi unaompa fursa kusimamia hata mwajiriwa bila kuathiri ajira yake.
  • Na kwa wale akina fulani katika shughuli za kijadi kuku ni moja ya zawadi au malipo kama mteja hana pesa.

No comments:

Post a Comment